Asasi Yetu

FAHAMU ZAIDI JUU YA ASASI YETU YA TAREO

TAREO ni kifupisho cha Tanzania Rural Empowerment Organization ,asasi isiyo  ya kiserikali,kidini wala yenye kutenegeza faida..Tareo iliazishwa mwaka 2000 na kupata usajili mwaka 2008 kwa Sheria ya uazishaji wa asasi zisizo za kiserikali (NGO) No;

Moja ya jukumu letu ni  kuwawezesha wakazi wa vijijini ki-elimu ,Technolojia, Afya na kuwashirikisha katika kutatua changamoto zinazo wakabili  ikiwa ni pamoja na ; Kuendeleza elimu; ufundi stadi na kutumia teknolojia ya Habari katika kujua na kutumia fursa zilizo Tanzania.

Baadhi ya huduma na miradi imefanikishwa na tasisi hii ikiwa ni pamoja na kuelimisha,kutoa huduma za kijamii,misaada na kuazisha vikundi na miradi endelevu kwa jamii na vikundi ; Uanzishaji wa miradi ya kuingiza kipato  vijijini, Mafunzo, Ushauri na huduma za, Masoko na Habari, na Huduma za mafunzo ya ajira na kujiajiri.

Shirika linatoa huduma zake kwa kupitia ofisi zake zilizopo Moshi ,kilimanjaro,Kimara Dar es salaam na Tanga pia kwa kutumia mtandao wake wa ofisi za vikundi zilizo kzribia kila mkoa hapa Tanzania Bara .

Shirika linfanya kazi na wadau wa ndani,nje na wafadhili wanao gharamia miradi ya wanachi inayo lenga kuondoa umaskini na kukuza elimu kwa watoto na vijana, kipato kwa  vijana na akina mama,ajira kwa vijana na jamii za vijijini  na pia matumzi ya TEHAMA katika kurahisha utendaji na kupata taarifa ndani na nje ya Tanzania.

FAHAMU ZAIDI JUU YA KAZI NA MIRADI YETU TUNAYO ENDESHA NA JAMII.

MIRADI YA ELIMU YA AWALI MIRADI YA TEHAMA (ICT) MIRADI YA AFYA NA MAJI

MIRAI YA UFUNDI NA AJIRA

MIRADI YA MAZINGIRA

TEHAMA-KWA WATOTOVIJIJINI
MIRADI YA VIJANA NA AJIRA

MIRADI YA AKINA MAMA
Miradi yetu na malengo yake kwa mtazamo
Utamaduni uliodumu tangu kale wa wa-Tanzania na mambo yote ya kimila yanayozunguka maisha ya kila mmoja kijini kwao TAREO ina amini kuwa yanatakiwa kutunzwa kwa ajili ya faida ya vizazi vijavyo (TUNA MAKABILA ZADI YA 120 TANZANIA).
Kupitia usaidizi wa mtu mmoja mmoja tunataka kusaidia watanzania wa vijijini kubadilika ,kuwa na maendeleo na  kutunza utamaduni wao.
Kupitia miradi imara na endelevu tukiyo aza nayo MAJENGO-KIJIJI CHA KYOMU, KATA ZA KAHE kunatakiwa kuwepo na vyanzo vipya vya mwazo na fedha kwa ajili kutunza na kuendeleza ukanda wa chini wa mlima KILIMANJARO(Sehemu za TAMBARARE).
Jamii ya WAKAHE inatakiwa kujiamulia yenyewe juu ya maisha yake ya baadae na vitu vyote muhimu vya kujiimarisha kimaisha.Miradi ifuatayo ya “ELIMU NA UJASIRIAMALI” imeanzishwa na jamii ya wakahe  wenyewe. Na sisi tukiwa kama marafiki wa jamii ya wakahe tunataka kusaidia watu hawa na utamaduni wao katika maisha yao ya kila siku ya kujipatia riziki.

Una maswali yoyote au msaada wa kimawazo?
Au unataka kuhusishwa katika miradi hii na jamii ya wakahe? –
Tafadhali wasiliana nasi kupitia barua pepe: info@nulltareo-tz.org
Au unataka kuchangia mradi wowote wa kuisadia KAHE”?

Miradi ya “kuongeza majengo Ya elimu na Ufundi stadi” (UJENZI):

Katika lugha ya ujumla ya “UJENZI” kuna miradi mbalimbali ya kuongeza na kuimarisha miradi elimu na mafunzo kwa watoto,vijana,akina mama na jamii nzima kama vile sehemu za kufundishai elimu ya awali,kuboresha majengo ya sgule za umma azilizopo, mfumo wa nishati ya jua na sehemu maalumu ya kupata huduma ya mtandao wa kumpyuta katika ofisi na sehemu za biashara za vijana . Kuboresha sehemu za utoaji huduma za afya haswa dispenasry zetu za Kyomu,Mwangaria,Kochakindo,Kahe,Oria,nk Hii pia itasaidia kujenga vyumba za watumishi,kuwekea vifaa mbalimbali ambavyo vinaweza kutumika na jamii katika kujisaidia katika miradi mingine ya ndani.

Soma kwa undani zaidi…

Miradi ya “kusaidi jamii isiyo na uwezo ” (Empowernment Projects):

Katika lugha ya ujumla ya usaidizi wa miradi ya kuisadia jamii  kuna miradi mbalimbali kwa kushirikiana na wadau wa nje na ndani (Asasi washirika wetu isiyo ya kiserikali ya hapa nchini) asasi ambayo inasaidia jamii. Kwa mfano tumeweza  kujenga na kuboresha huduma za maji , na mifumo ya maji katika maeneo ya Shule ya msingi Majengo,Shule ya msingi Soko,na jamii zinazozunguka maeneo haya . Kwa kushirikiana na asasi washirika huwa tunaandaa safari za kutembelea maeneo hayo ,kuona changamoto na na kuwapa nafasi wadau na wenyeji wa eneo hilo kueleza chamanamoto zao na kuependekeza namana wanavyo fikiri linaweza tatulika.

Pia tuna washirikisha wadau wetu kuleta wafanayakazi wa kujitolea na vifaa vya kutolea elimu au kufundishia katika maeneo hayo na shule za msingi za eneo husika ili kutoa fursa ya jamii na wanafunzi kutoka jamii hii  msaada wa mafunzo mbalimbali ambayo ni endelevu.

Soma kwa undani zaidi…

Mradi wa “udhamini wa kielimu” (Malipo ya masomo na Shule):

Kuna uwepo wa shule chache sana katika eneo hili kubwa la ukanda wa KAHE na vijijini kwa ujumla. Shule hizi ili ziwe na ubora, mazingira mazuri na kutoa elimu bora zinahitaji msaada toka mashirika mbalimbali pamoja ni za  serikali ya Tanzania.
Japokuwa serikali ya Tanznaia imeondoa ulipaji wa ada shule zote za msingi za serikali ili watoto wote waende shule, lakini bado kuna shida kwa sababu kumpeleka mtoto shule kuna gharama zake, watoto wanatakiwa wawe na sare za shule, ambazo hazilipwi na serikali, na pia wanatakiwa wanunue vitabu, madaftari na kalamu na hata wakati mwingine tunahitaji kuboresha mazingira ya shule hizi.

Hii inasababisha familia nyingi maskini za vijijini na ukanda wa chini  kutokuwapeleka shule watoto wao kwa sababu hawawezi kumudu gharama hizi. Au pia wakiamua kupeleka watoto shule hupeleka watoto wa kiume tu na si wa kike.
Kwa sababu hii watoto wengi wa kike wanaotaka elimu hukosa fursa hii na kujikuta katika mazingira mengine. Kwa hiyo basi sisi “TAREO” tunataka kusaidia wasichana wa kikahe kupitia ufadhili ambao utawawezesha kujiunga na shule kwa ajili ya kupata elimu ya awali,msingi,secondari na hata chuo.

Miaka michache iliyo pita kupitia ufadhili wa shirika la Kijerumani (AKO) tuliweza kusadia zaidi ya wanafunzi 56 kusoma msingi,sekondari(Shule ya sekondari Ghona) na hatimae wengine kujiunga na Chuo cha kilimo na mifugo mwangaria(Chuo hicho kilisitshwa kwa sababu zilizo nje ya uwezo wetu)

P225.JPG

Soma kwa undani zaidi…

Mradi wa “KIPATO ENEDELEVU KWA AKINA MAMA” (Tunakuwa group):

Kuna familia nyingi za ijiji vya Kyomu,Ghona,Soko,Kochakindo,Mwangaria… ambazo akina mama wengi hawajui nini cha kufanya ili kuongea kipato cha familia .Mika michache iliyo pita ukanda wa KAHE ulipoteza mifugo yao kutokana na ukame au magonjwa ya mifugo. Kutokana na kuwepo kwa eneo tambarare, mito kukauka na kuwa na neema ya kupata maji ya visima vya kuchimba kwa mikono ,karibia kila kijiji kiliazisha mashamaba ya umwagiliaji .Mradi huu ujulikanao kama “Kilimo cha umwagiliaji ukanda wa chini” ukiwezesha mashamba yaliyo kaa muda mrefu bila kutumia kuaza uzalishaji. Hii ilitoa fursa yaajiara kubwa kwa akina mama na kuweza kujipatia kipato either kwa kulima au kufanya kazi katika mashamaba ya mahindi,maharage,nyaynya,vitunu,hoho…..nk. Kutokana na kila kijiji kimejaribi kuunda kikundi cha akaina mama na karibia kila kitongoji kna vikundi hivi.
Hapa MTAA WA MAJENGO-KIJIJI CHA KYOMU kwa kushirikiana na shirika la KIltech la kimarekani waliweza azisha vikundi madhubiti amabayo vipo kataka hali ya juu sana kwenye kuingiza kipato na kusadia elimu ya watotot,familia na jamii nzima ya KAHE.

   

Soma kwa undani zaidi…

Miradi ya “Kilimo na Usagaji nafaka ” (Agribusiness):

Kupitia miradi hii, katika duka la wamasai, jamii ya wanawake wa kimasai kutoka wilaya ya Simanjiro wanaweza kuuza bidhaa zao za kazi za mikono katika duka hili kupitia miradi ya “enkaina-e-retoto”, bidhaa kama shanga, mikufu na mikanda ya ngozi inayotengezwa na mali ghafi asili. Ambapo wanaziweka nakshi ya rangi mbalimbali. Baadhi ya bidhaa zitokanazo na chai asilia iliyochumwa pia zinatakiwa kupatikana katika duka dogo la wamasai kwenye makao makuu ya enkaina-e-retoto’’ katika eneo la Loiborsoit A.
Bidhaa za asili kutoka ulaya na nyingine (zilizotengenezwa Tanzania) zinaweza kununuliwa pia katika hili duka la bidhaa za mikono kwa kuongezea tunapenda kuuza vijarida na vitabu vihusuvyo utamaduni wa jamii ya kimasai kwa wageni wetu.
Faida zinazopatikana zinarudi kusaidia miradi mingine inayoweza kujiendeleza yenyewe umasaini.

Soma kwa undani zaidi…

Mradi wa “Maji na usafi mashuleni” (WASH PROJECT):

Mradi ulitokana na wazo kwamba watoto wengi wa shule za msingi hawana mfumo mzuri wa maji safi na taka na pia kuto nawa mikono bada ya kutoka chooni.TAREO kushirikiana na asasi ya Kimataiafa (AYANA INTERNATIONAL) tumeweza kuweka mifano ya sehemu za unawaji mikona na kuhamasisha watoto wa shule za msingi kubuni miradi midogo midoga ya usafi mashuleni

Tuanatarajia tukipata wadau wa kuasidia mradi huu,tuweke mashindano ya usafi,utuzaji mazingira na utumiaji wa taka kwa maendeleo mashuleni na majumbani.

Kite Dar es Salaam on Twitter: "Our volunteers from wash project ...

Getting Water to Women: AMREF's Mkuranga District WASH Project ...

 

Soma kwa undani zaidi…

Mradi wa “Maktaba ya Jamii Vijijini ” (Majengo Community Library):

Wakazi wengi wa Vijijini hususani wa ukanda wa tambarare kama KAHE ikiwa ni pamoja wanafunzi wengi wanao soma msingi na sekondari wamekuwa wakipata changamoto ya sehemu ya kujisomea wakati wa jioni au likizo.
TAREO tuna amaini kuwa kusoma ni sehemu ya kuongeza maarifa hivyo tumeazisha makataba na kwa sasa tuna mahitaji ya vijitabu vidogo,majarida, magazeti na hata internet kwa ajili ya kujua na kujifunza masomo na kazi zetu hususani kilimo,ufugaji na biashara. Tuna mikakati pia ya kuandika vitabu vya lugha mbalimbali ndogondogo zilizopo TANZANIA na moja wapo ni maneno katika lugha ya Kikahe  ili kuweza kuhifadhi kwa ajili ya vizazi vijavy.

Kwa ushirikiano na wana jamii watokao KAHE na marafiki wengine kutoka pande mbalimbali za dunia tunaweza kuandaa andiko la kwanza juu ya suala la lugha,mila,desturi na maisha ya WAKAHE na makabila mengine..

Soma kwa undani zaidi…

Miradi ya “Elimu ufundi mtandao ” (VET-DIGITAL SKILLS PROGRAM):

Mnamo mwaka 2005 tuliweza kuanzisha Chuo cha ufundi stadi cha elimu ya Computer na teknolojia-MOSHI INSTITUTE OF TECHNOLOGY-MIT).Chuo na tasisis hii ipo Moshi mjini na kinaendesha mafunzo ya TEHAMA chini ya VETA .

Baade tuliweza azisha kituo cha mafunzo ya vijana Himo(HIMO YOUTH AND ICT CENTRE)

Na kupitia uzamini wa shirika kubwa dunianai tuliazisha shule ya awali ya watototo na vijana kujifunza kutumia TEHAM(MAJENGO KIDS AND YOUTH TECHNOLOGY SCHOOL) .
Washirika wetu siku zote wamekuwa wakifurahia matokeo makubwa ya vituo hivu vya elimu na mafunzo ,na kushirikiana na wazamini tumekuwa tukichukua wanafunzi wa ukanda wa chini pamoja na wale wanao toka vijijini kujiunga mafunzo haya.
Kila siku tunajaribu kufanya gharama za mafunzo na kiutawala ziwe ndogo kadri iwezekanavyo ili tuweze kusadia watu wengi zaidi kwa gaharama nafuu au bure kabisa. Uwekaji wa nishati ya jua na mtandao wa kompyuta pia nao ni muhimu kwa miradi mingine inayoendelea haswa kule vijijini na TIGO pia wameweza shiriki hili na ktufungia matandao katiaka shule ya awali a MAJENGO.

Soma kwa undani zaidi…

Mawazo ya miradi mipya:

Je una swali lolote ama ushauri kwa ajili ya mawazo mapya ya miradi ya kujiendesha katika eneo la jamii za VIJIJINI. Tunataka kuwa makini katika utatuzi wa matatizo yaliyopo katika jamii za watu wa chini pamoja na kusaidia mazingira ya huduma muhimu ikiwa ni pamoja kuhakikisha upatiknaji wa taarifa na matumizi ya TEHAMA. Muda wote tupo wazi kwa mawasiliano na kupokea wagemi wa ndani na njea. Na pia kama unataka kuja kuona miradi yetu, ama unataka kuhusishwa katika miradi yetu inayoendelea unakaribishwa sanai.

Pia  kama una maoni ya kiutendaji juu ya miradi yetu inayoendelea. Washirika wetu “OUR TEAM” wapo tayari muda wote kufanya kazi pamoja na asasi zingine na pia kutoa msaada wa namana ya kushiriki katika miradi au jamii yenye uhitaji.